Tamthilia hutofautiana na riwaya na hadithi fupi kutokana na muundo wake. Tamthilia hutegemea mazungumzo na uwasilishaji wa jukwaani kuupitisha ujumbe wake. Mwandishi wa tamthilia, tofauti na wengine, analazimika kuwazia:
- uigizaji
- matumizi ya maleba
- matumizi ya taa na mwangaza
- sauti za wahusika au vifaa vingine
- matumizi ya kimya
- ngoma na uchezaji
- kuwepo kwa wahusika mbele ya hadhira na jukwaa lenyewe.
Tamthilia huwa na kaida au kanuni maalum ambazo hazipatikani katika tanzu nyingine za kifasihi. kanuni hizi zinahusiana na:
- matumizi ya usemaji kando
- ugawaji wa sehemu mbalimbali kwenye maonyesho au matendo
- matumizi ya mbinu ya ujifanyaji- mhusika mmoja anapojifanya kuwa mhusika mwingine
- matumizi ya mkarara au kipokeo kinachorudiwarudiwa
- wahusika wanaojizungumzia wao
- wahusika kuwasiliana na hadhira
- matumizi ya ngoma, nyimbo na uimbaji kuongeza uzito.
No comments:
Post a Comment